Latest News

Tuesday, October 18, 2016

Wafanyabiashara Soko Kuu Iringa walalamika kuzuiwa kipimo cha Ndoo

Baadhi ya Wafanya biashara wa katika soko kuu Manispaa ya iringa wamelalamikia tabia inayofanywa na baadhi ya viongozi wa mamlaka ya vipimo kuwazuia kutumia kipimo cha ndoo katika biashara zao.
 
Wakizungumza na nuru fm wafanya biashara hao wamedai kuwa wamekuwa wakizuiwa kutumia ndoo ndogo katika kupima vitunguu kama kipimo cha mzani wakati kuna wanyabiashara wengine nje ya soko hilo wanatumia njia hiyo.

 
Aidha wafanya biashara hao wamesema kuwa tangu kuanza kwa biashara hiyo hawajawai pokea taarifa kutoka kwenye uongozi wowote kuwa kuna mabadiliko katika upimaji wa bidhaa zao.

No comments:

Post a Comment