Latest News

Tuesday, October 11, 2016

Polisi wajeruhi watuhumiwa wa ujambazi Dar

Watuhumiwa wawili kati ya watano wa ujambazi wamejeruhiwa katika majibizano ya risasi na jeshi la polisi na kutiwa mbaroni katika eneo la Vingunguti jijini Dar es Salaam,baada ya kueleza lilikuwa jaribio la kupora fedha katika kiwanda kimoja. Katika tukio hilo watuhumiwa watatu wamefanikiwa kutoroka.Taarifa hiyo imetolewa na kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, kamanda Simon Sirro.“Polisi wa jiji la Dar es Salaam waliwahi eneo na wakafanya mtego na kweli bahati nzuri walifanikiwa,kabla wale majambazi hawajafanya tukio walifanikiwa kuwarushia risasi,kwa maana ya kutaka wasimame, lakini na wao hawakukubali kusimama,” alieleza Sirro.“Kwahiyo polisi walipiga risasi juu na walipoona mwisho wa siku wakapotea, wakaweza kuwapiga risasi majambazi wawili na walipokwenda kuwapekua ndio walikuta hii silaha ya aina ya MARK IV.”

No comments:

Post a Comment