Leo msanii #Richmavoko amesainiwa rasmi kwenye label ya wasafi ya WCB Inayoongozwa na Diamond Platnumz, hivyo anaungana na Rayvanny na Harmonize katika kuendelea kung'arisha label hiyo, sasa hii ni video aliyoiachia baada ya kusainishwa rasmi wasafi inaitwa Ibaki stori.
Karibu kwa mara nyingine kutizama video mpya ya Bill Nas ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Demu gani ambayo amemshirikisha Barnaba Classic.
Video hii haina taarifa rasmi kuhusu kuachiwa ila baada kupita huku na kule nimeweza kuibahatisha nikaona ni vema nikuletee uweze kuitizama kisha uache maoni yako.
Video imesimamiwa na kampuni ya LFLG na audio imefanywa na Mesen Selekta pale Defatality.
Karibu kutizama video mpya ya wimbo wa Bill Nas unaoitwa Chafu pozi ambao tayari audio yake imekamata nafasi za juu kwenye vituo mbali mbali vya redio.
Tizama video mpya ya G Nako aliwashirikisha Chin Beez na Nikki wa pili inaitwa Arosto ambayo imeongozwa na Hanscana na audio imefanywa na Lufa pale Switch Records.
Karibu kutizama video mpya ya msanii Alikiba inaitwa Aje ambayo amemshirikisha M.I. Video imeongozwa na phenomenal Director Meji chini ya uongozi wa ROCKSTAR4000.