Mbunge wa
zamani wa jimbo la Moshi mjini, na mwenyekiti wa chama cha demokrasia na
maendeleo, Chadema mkoani Kilimanjaro, Philemon Ndesamburo, amefariki dunia
muda mfupi baada ya kufika ofisini kwake, jana asubuhi, ambapo alikuwa
akijiandaa na majukumu yake ya kila siku.
Taarifa za
mapema zinaeleza kuwa mzee Ndesamburo amefariki jana jumatano majira ya saa nne
asubuhi akiwa katika kitengo cha wagonjwa wa dharula katika Hospitali ya KCMC Moshi, ambapo alipelekwa kwaajili ya matibabu, baada ya hali yake kubadilika ghafla mara
baada tu ya kufika ofisini.
Katibu wa
Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Bazil Lema amesema mwili wa aliyekuwa mbunge wa
jimbo la Moshi mjini Phillemon Ndesamburo unafanyiwa uchunguzi ili kubaini
chanzo cha kifo chake cha ghafla na kuongeza kuwa Ndesamburo alifika ofisini
kwake asubuhi kama ilivyo kawaida yake lakini aliugua ghafla mnamo
saa nne asubuhi.
Mstahiki
Meya wa manispaa ya Moshi, Raymond Mboya, ameeleza kuwa moja ya majukumu
aliyokuwa nayo Marehemu siku ya jana ni pamoja na kukabidhi hundi ya
rammbirambi, kwa wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Luck Vicent, ya
jijini Arusha.
Mtaalamu wa
magonjwa ya binadamu na ngozi wa hospitali ya KCMC Profesa Elisante Masenga,
ameelezea sababu za kifo cha mzee Ndesamburo
, huku Rais wa
Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, ametuma salamu za
rambi rambi kwa familia ya marehemu Philemon Ndesamburo, viongozi wa chama cha
demokrasia na maendeleo Chadema, pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wote
walioguswa na kifo hicho.

No comments:
Post a Comment